10. “Kuta za matofali zimeangukalakini sisi tutazijenga kwa mawe yaliyochongwa!Nyumba za boriti za mikuyu zimeharibiwalakini mahali pake tutajenga za mierezi.”
11. Basi, Mwenyezi-Mungu atawaletea wapinzanina kuwachochea maadui zao.
12. Waaramu upande wa mashariki,Wafilisti upande wa magharibi,wamepanua vinywa vyao kuimeza Israeli.Hata hivyo, hasira yake haijatulia,bado ameunyosha mkono wake.
13. Ingawa aliwaadhibu watu,hawakumrudia Mwenyezi-Mungu wa majeshi.
14. Basi kwa muda wa siku moja tu,Mwenyezi-Mungu atakata katika Israeli vichwa na mikia,tawi la mtende na nyasi:
15. Vichwa ndio wazee na waheshimiwa,mikia ndio manabii wafundishao uongo.
16. Wale wanaoongoza watu hawa wamewapotosha,na hao wanaoongozwa nao wamepotoka.