1. “Wewe Beli umeanguka;Nebo umeporomoka.Wakati mmoja watu walibeba sanamu zenu.Sasa wanazibeba mgongoni mwa wanyama,hao wanyama wachovu wamelemewa.
2. Nyinyi mmeanguka na kuvunjika,hamwezi kuviokoa vinyago vyenu;nyinyi wenyewe pia mtapelekwa uhamishoni!
3. “Sikilizeni enyi wazawa wa Yakobo,nisikilizeni enyi mabaki ya watu wangu wa Israeli.Mimi niliwatunzeni tangu mlipozaliwa;niliwabebeni tangu tumboni mwa mama yenu.