8. Humo kutakuwa na barabara kuu,nayo itaitwa “Njia Takatifu.”Watu najisi hawatapitia humo,ila tu watu wake Mungu;wapumbavu hawatadiriki kuikanyaga,
9. humo hakutakuwa na simba,mnyama yeyote mkali hatapitia humo,hao hawatapatikana humo.Lakini waliokombolewa ndio watakaopita humo.
10. Waliokombolewa na Mwenyezi-Mungu watarudi,watakuja Siyoni wakipiga vigelegele.Watakuwa wenye furaha ya milele,watajaliwa furaha na shangwe;huzuni na kilio vitatoweka kabisa.