14. dhidi ya milima yote mirefu,dhidi ya vilima vyote vya juu;
15. dhidi ya minara yote mirefu,dhidi ya kuta zote za ngome;
16. dhidi ya meli zote za Tarshishi,na dhidi ya meli zote nzuri.
17. Kiburi chote cha watu kitakomeshwa,majivuno ya kila mtu yatavunjwa.Na Mwenyezi-Mungu peke yake atatukuzwa siku hiyo.
18. Vinyago vyote vya miungu vitatoweka kabisa.
19. Ingieni katika mapango miambani,katika mashimo ardhini,kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,mbali na utukufu wa enzi yake,atakapokuja kuitia hofu dunia.