26. Huu ndio uamuzi wake Mwenyezi-Mungukuhusu dunia yote;hii ndiyo adhabu atakayotoajuu ya mataifa yote.
27. Kama Mwenyezi-Mungu wa majeshi ameamua,nani atakayeweza kubatilisha uamuzi wake?Kama amepania kutoa adhabu,ni nani atakayempinga?
28. Mwaka alipofariki mfalme Ahazi, Mungu alitoa kauli hii:
29. “Msishangilie enyi Wafilisti wote,kwamba Ashuru, fimbo iliyowapiga, imevunjika;maana, nyoka wa kawaida atazaa nyoka mwenye sumu,na nyoka mwenye sumu atazaa joka lirukalo.
30. Wazaliwa wa kwanza wa maskini watashiba,na fukara watakaa kwa usalama.Lakini chipukizi wenu nitawaua kwa njaa;na yeyote wenu atakayebaki nitamuua.
31. Piga yowe ewe lango; lia ewe mji;yeyuka kwa hofu ewe nchi yote ya Filistia.Maana moshi wa askari waja kutoka kaskazini,wala hakuna atakayechelewa katika majeshi yake.”
32. Basi watapewa jibu gani wajumbe wa taifa hilo?Wataambiwa: Mwenyezi-Mungu ameijenga imara Siyoni,na maskini wa watu wake watakimbilia usalama huko.