10. Alisema hivyo kwa sababu alijua wazi kwamba makuhani wakuu walimkabidhi Yesu kwake kwa sababu ya wivu.
11. Lakini makuhani wakuu wakawachochea watu wamwombe Pilato awafungulie Baraba.
12. Pilato akawauliza tena, “Basi, sasa mwataka nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
13. Watu wote wakapaza sauti tena: “Msulubishe!”