Agano la Kale

Agano Jipya

Neh. 9:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Hata siku ya ishirini na nne ya mwezi huo wana wa Israeli wakawa wamekusanyika, wakifunga, wenye kuvaa magunia, na kujitia udongo vichwani.

2. Waliokuwa wa wazao wa Israeli wakajitenga na wageni wote, wakasimama, wakaziungama dhambi zao, na maovu ya baba zao.

3. Basi wakasimama mahali pao, wakasoma katika kitabu cha torati ya BWANA, Mungu wao, muda wa robo ya siku; na robo nyingine wakaungama, wakamwabudu BWANA, Mungu wao.

Kusoma sura kamili Neh. 9