Agano la Kale

Agano Jipya

Neh. 7:61-69 Swahili Union Version (SUV)

61. Na hawa ndio watu waliokwea kutoka Tel-mela, na Tel-harsha, na Kerubu, na Adani, na Imeri; walakini hawakuweza kuonyesha mbari za baba zao, wala kizazi chao, kwamba walikuwa wa Israeli;

62. Wana wa Delaya, wana wa Tobia, wana wa Nekoda, mia sita na arobaini na wawili.

63. Tena katika makuhani; Wana wa Habaya, wana wa Hakosi, wana wa Barzilai, yule aliyeoa mmojawapo binti Barzilai, Mgileadi, akaitwa kwa jina lao.

64. Hao waliitafuta orodha yao miongoni mwa wale waliohesabiwa kwa nasaba, wasionekane; kwa hiyo walihesabiwa kuwa na unajisi.

65. Na huyo Tirshatha akawaambia kwamba wasile katika vile vitu vitakatifu sana, hata atakaposimama kuhani mwenye Urimu na Thumimu.

66. Basi hilo kusanyiko lote zima, jumla yake ilikuwa watu arobaini na mbili elfu na mia tatu na sitini,

67. tena zaidi ya hao, kulikuwa na watumishi wao waume kwa wake, ambao walikuwa elfu saba na mia tatu na thelathini na saba; kisha walikuwa na waimbaji waume kwa wake mia mbili arobaini na watano.

68. Farasi zao walikuwa mia saba thelathini na sita; nyumbu zao, mia mbili arobaini na watano;

69. ngamia zao, mia nne thelathini na watano; punda zao, elfu sita na mia saba na ishirini.

Kusoma sura kamili Neh. 7