Agano la Kale

Agano Jipya

Neh. 7:61-64 Swahili Union Version (SUV)

61. Na hawa ndio watu waliokwea kutoka Tel-mela, na Tel-harsha, na Kerubu, na Adani, na Imeri; walakini hawakuweza kuonyesha mbari za baba zao, wala kizazi chao, kwamba walikuwa wa Israeli;

62. Wana wa Delaya, wana wa Tobia, wana wa Nekoda, mia sita na arobaini na wawili.

63. Tena katika makuhani; Wana wa Habaya, wana wa Hakosi, wana wa Barzilai, yule aliyeoa mmojawapo binti Barzilai, Mgileadi, akaitwa kwa jina lao.

64. Hao waliitafuta orodha yao miongoni mwa wale waliohesabiwa kwa nasaba, wasionekane; kwa hiyo walihesabiwa kuwa na unajisi.

Kusoma sura kamili Neh. 7