Agano la Kale

Agano Jipya

Mhu. 6:7-11 Swahili Union Version (SUV)

7. Kazi yote ya binadamu ni kwa kinywa chake,Walakini hata hivyo nafsi yake hashibi.

8. Kwa maana mwenye hekima hupata faida gani kuliko mpumbavu? Au maskini ana nini kuliko yeye ajuaye kwenda mbele ya walio hai?

9. Heri kuona kwa macho,Kuliko kutanga-tanga kwa tamaa.Hayo nayo ni ubatili, na kujilisha upepo.

10. Na awe kitu cho chote, aliitwa jina lake zamani za kale, naye amejulikana kuwa ndiye mwanadamu; wala hawezi kabisa kushindana na yeye aliye na uwezo kuliko yeye mwenyewe.

11. Basi, kwa kuwa kuna mambo mengi yaongezayo ubatili, mwanadamu hufaidiwa nini?

Kusoma sura kamili Mhu. 6