Agano la Kale

Agano Jipya

Mhu. 6:1-8 Swahili Union Version (SUV)

1. Kuna baa nililoliona mimi chini ya jua, nalo linawalemea wanadamu kwa uzito;

2. mtu aliyepewa na Mungu mali, ukwasi, na heshima, hata asipungukiwe na kitu cho chote kwa nafsi yake, katika yote anayoyatamani walakini Mungu hamwezeshi kula katika hizo; bali mgeni hula. Hayo ndiyo ubatili hasa, nayo ni ugonjwa mbaya.

3. Mtu akizaa watoto mia, akaishi miaka mingi, nazo siku za maisha yake ni nyingi, lakini nafsi yake haikushiba mema; tena ikiwa, zaidi ya hayo, amekosa maziko; mimi nasema, Heri mimba iliyoharibika kuliko huyo;

4. yaani, hiyo huja katika ubatili, na huenda gizani, nalo jina lake limefunikwa giza;

5. tena, haikuliona jua wala kulifahamu; basi, hii imepata kustarehe kuliko yule;

6. naam, ajapoishi miaka elfu mara mbili, asijiburudishe kwa mema; je! Wote hawaendi mahali pamoja?

7. Kazi yote ya binadamu ni kwa kinywa chake,Walakini hata hivyo nafsi yake hashibi.

8. Kwa maana mwenye hekima hupata faida gani kuliko mpumbavu? Au maskini ana nini kuliko yeye ajuaye kwenda mbele ya walio hai?

Kusoma sura kamili Mhu. 6