Agano la Kale

Agano Jipya

Mhu. 6:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Kuna baa nililoliona mimi chini ya jua, nalo linawalemea wanadamu kwa uzito;

2. mtu aliyepewa na Mungu mali, ukwasi, na heshima, hata asipungukiwe na kitu cho chote kwa nafsi yake, katika yote anayoyatamani walakini Mungu hamwezeshi kula katika hizo; bali mgeni hula. Hayo ndiyo ubatili hasa, nayo ni ugonjwa mbaya.

3. Mtu akizaa watoto mia, akaishi miaka mingi, nazo siku za maisha yake ni nyingi, lakini nafsi yake haikushiba mema; tena ikiwa, zaidi ya hayo, amekosa maziko; mimi nasema, Heri mimba iliyoharibika kuliko huyo;

4. yaani, hiyo huja katika ubatili, na huenda gizani, nalo jina lake limefunikwa giza;

5. tena, haikuliona jua wala kulifahamu; basi, hii imepata kustarehe kuliko yule;

Kusoma sura kamili Mhu. 6