15. Yaliyopotoka hayawezi kunyoshwa,Wala yasiyokuwapo hayahesabiki.
16. Nikatafakari nikisema, Nimejipatia hekima nyingi kupita wote walionitangulia katika Yerusalemu; naam, moyo wangu umeona kwa wingi hekima na maarifa.
17. Nikatia moyo wangu ili kuijua hekima, na kujua wazimu na upumbavu; nikatambua ya kwamba hayo yote nayo ni kujilisha upepo.
18. Yaani,Katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni;Naye aongezaye maarifa huongeza masikitiko.