Agano la Kale

Agano Jipya

Mhu. 1:15-18 Swahili Union Version (SUV)

15. Yaliyopotoka hayawezi kunyoshwa,Wala yasiyokuwapo hayahesabiki.

16. Nikatafakari nikisema, Nimejipatia hekima nyingi kupita wote walionitangulia katika Yerusalemu; naam, moyo wangu umeona kwa wingi hekima na maarifa.

17. Nikatia moyo wangu ili kuijua hekima, na kujua wazimu na upumbavu; nikatambua ya kwamba hayo yote nayo ni kujilisha upepo.

18. Yaani,Katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni;Naye aongezaye maarifa huongeza masikitiko.

Kusoma sura kamili Mhu. 1