Agano la Kale

Agano Jipya

Kum. 23:22-25 Swahili Union Version (SUV)

22. Lakini ukijizuia usiweke nadhiri, haitakuwa dhambi kwako.

23. Yaliyotoka midomoni mwako yashike kuyafanya; kwa mfano wa ulivyomwekea nadhiri BWANA, Mungu wako, ni sadaka ya hiari uliyoahidi kwa kinywa chako.

24. Uingiapo katika shamba la mizabibu la jirani yako, utaweza kula zabibu za kukushibisha, kama upendavyo; ila usitie katika chombo chako.

25. Uingiapo katika mmea wa jirani yako waweza kuyapurura masuke kwa mkono wako; ila usisongeze mundu katika mmea wa jirani yako.

Kusoma sura kamili Kum. 23