Agano la Kale

Agano Jipya

Hos. 9:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Usifurahi, Israeli, kwa sababu ya furaha, kama hao mataifa; kwa kuwa umezini juu ya Mungu wako, umependa ujira katika kila sakafu ya nafaka.

2. Sakafu na shinikizo hazitawalisha, na divai mpya itampungukia.

3. Hawatakaa katika nchi ya BWANA; lakini Efraimu atarudi Misri, nao watakula chakula kinajisi katika Ashuru.

4. Hawatammiminia BWANA divai, wala hazitampendeza sadaka zao; mkate wao utakuwa kama chakula cha matanga kwao; wote watakaokila watatiwa unajisi; kwa maana mkate wao utakuwa kwa shauku zao; hautaingia katika nyumba ya BWANA.

5. Mtafanya nini katika siku ya mkutano wa idi, na katika siku ya karamu ya BWANA?

Kusoma sura kamili Hos. 9