Agano la Kale

Agano Jipya

Hos. 8:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Tia baragumu kinywani mwako. Kama tai, anakuja juu ya nyumba ya BWANA; kwa sababu wamelihalifu agano langu, wameiasi sheria yangu.

2. Watanililia, Mungu wangu, sisi Israeli tunakujua.

3. Israeli ameyatupa yaliyo mema; adui watamfuatia.

4. Wamesimamisha wafalme, lakini si kwa shauri langu; wamejifanyia wakuu, lakini nalikuwa sina habari; kwa fedha yao na dhahabu yao wamejifanyizia sanamu, kusudi wakatiliwe mbali.

5. Amemtupa ndama yako, Ee Samaria; hasira yangu imewaka juu yao; siku ngapi zitapita kabla ya hao kupata hali isiyo na hatia?

6. Maana katika Israeli kimetokea hata na kitu hiki; fundi ndiye aliyekifanya, nacho si mungu kamwe; naam, ndama ya Samaria itavunjika vipande vipande.

Kusoma sura kamili Hos. 8