Agano la Kale

Agano Jipya

Hos. 8:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Tia baragumu kinywani mwako. Kama tai, anakuja juu ya nyumba ya BWANA; kwa sababu wamelihalifu agano langu, wameiasi sheria yangu.

2. Watanililia, Mungu wangu, sisi Israeli tunakujua.

3. Israeli ameyatupa yaliyo mema; adui watamfuatia.

4. Wamesimamisha wafalme, lakini si kwa shauri langu; wamejifanyia wakuu, lakini nalikuwa sina habari; kwa fedha yao na dhahabu yao wamejifanyizia sanamu, kusudi wakatiliwe mbali.

Kusoma sura kamili Hos. 8