Agano la Kale

Agano Jipya

Hos. 12:1-8 Swahili Union Version (SUV)

1. Efraimu hujilisha upepo, na kuandamana na upepo wa mashariki; haachi kuongeza uongo na uharibifu; nao wafanya agano na Ashuru, na mafuta huchukuliwa kwenda Misri.

2. BWANA naye ana mateto na Yuda, naye atamwadhibu Yakobo kwa kadiri ya njia zake; kwa kadiri ya matendo yake atamlipa.

3. Tumboni alimshika ndugu yake kisigino;Na alipokuwa mtu mzima alikuwa na uwezo kwa Mungu;

4. Naam, alikuwa na uwezo juu ya malaikaAkashinda; alilia, na kumsihi;Alimwona huko Betheli, naye akasema nasi huko;

5. Naam, BWANA, Mungu wa majeshi;BWANA ndilo kumbukumbu lake.

6. Basi, mrudie Mungu wako; shika fadhili na hukumu; ukamngojee Mungu wako daima.

7. Ni mchuuzi, mizani ya udanganyifu i mkononi mwake; anapenda kudhulumu.

8. Naye Efraimu alisema, Kweli nimekuwa tajiri, nimejipatia mali nyingi; katika kazi zangu zote hawataona kwangu uovu wo wote uliokuwa dhambi.

Kusoma sura kamili Hos. 12