1. Lisikieni neno hili nilitamkalo liwe maombolezo juu yenu, enyi nyumba ya Israeli.
2. Bikira wa Israeli ameanguka;hatainuka tena;Ameangushwa katika nchi yake;hakuna mtu wa kumwinua.
3. Kwa kuwa Bwana MUNGU asema hivi; Mji uliotoka nje wenye watu elfu, utasaziwa watu mia, na mji uliotoka wenye watu mia, utasaziwa watu kumi, kwa nyumba ya Israeli.