Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 7:43-52 Swahili Union Version (SUV)

43. Basi kukaingia matengano katika mkutano kwa ajili yake.

44. Baadhi yao wakataka kumkamata, lakini hakuna mtu aliyenyosha mikono yake ili kumshika.

45. Basi wale watumishi wakawaendea wakuu wa makuhani na Mafarisayo. Nao wakawaambia, Mbona hamkumleta?

46. Wale watumishi wakajibu. Hajanena kamwe mtu ye yote kama huyu anavyonena.

47. Basi Mafarisayo wakawajibu, Je! Ninyi nanyi mmedanganyika?

48. Ni nani katika wakuu amwaminiye, au katika Mafarisayo?

49. Lakini makutano hawa wasioifahamu torati wamelaaniwa.

50. Akawaambia Nikodemo, (naye ni yule aliyemwendea zamani, maana ni mmoja wao),

51. Je! Torati yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza, na kujua atendavyo?

52. Wakajibu, wakamwambia, Je! Wewe nawe umetoka Galilaya! Tafuta, ukaone ya kuwa kutoka Galilaya hakutokea nabii.

Kusoma sura kamili Yn. 7