Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 7:4-12 Swahili Union Version (SUV)

4. Kwa maana hakuna mtu afanyaye neno kwa siri, naye mwenyewe ataka kujulikana. Ukifanya mambo haya, basi jidhihirishe kwa ulimwengu.

5. Maana hata nduguze hawakumwamini.

6. Basi Yesu akawaambia, Haujafika bado wakati wangu; ila wakati wenu sikuzote upo.

7. Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi; bali hunichukia mimi, kwa sababu mimi naushuhudia ya kuwa kazi zake ni mbovu.

8. Kweeni ninyi kwenda kula sikukuu; mimi sikwei bado kwenda kula sikukuu hii, kwa kuwa haujatimia wakati wangu.

9. Naye alipokwisha kuwaambia hayo, alikaa vivi hivi huko Galilaya.

10. Hata ndugu zake walipokwisha kukwea kuiendea sikukuu, ndipo yeye naye alipokwea, si kwa wazi bali kana kwamba kwa siri.

11. Basi Wayahudi wakamtafuta kwenye sikukuu, wakasema, Yuko wapi yule?

12. Kukawa na manung’uniko mengi katika makutano juu yake. Wengine wakasema, Ni mtu mwema. Na wengine wakasema, Sivyo; bali anawadanganya makutano.

Kusoma sura kamili Yn. 7