Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 7:15-20 Swahili Union Version (SUV)

15. Wayahudi wakastaajabu wakisema, Amepataje huyu kujua elimu, ambaye hakusoma?

16. Basi Yesu akawajibu, akasema, Mafunzo yangu si yangu mimi, ila ni yake yeye aliyenipeleka.

17. Mtu akipenda kuyatenda mapenzi yake, atajua habari ya yale mafunzo, kwamba yatoka kwa Mungu, au kwamba mimi nanena kwa nafsi yangu tu.

18. Yeye anenaye kwa nafsi yake tu hutafuta utukufu wake mwenyewe; bali yeye anayetafuta utukufu wake aliyempeleka, huyo ni wa kweli, wala ndani yake hamna udhalimu.

19. Je! Musa hakuwapa torati? Wala hakuna mmoja wenu aitendaye torati. Mbona mnatafuta kuniua?

20. Mkutano wakajibu, Ama! Una pepo! Ni nani anayetafuta kukuua?

Kusoma sura kamili Yn. 7