Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 7:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Na baada ya hayo Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya; maana hakutaka kutembea katika Uyahudi, kwa sababu Wayahudi walikuwa wakitafuta kumwua.

2. Na sikukuu ya Wayahudi, Sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu.

3. Basi ndugu zake wakamwambia, Ondoka hapa, uende Uyahudi, wanafunzi wako nao wapate kuzitazama kazi zako unazozifanya.

4. Kwa maana hakuna mtu afanyaye neno kwa siri, naye mwenyewe ataka kujulikana. Ukifanya mambo haya, basi jidhihirishe kwa ulimwengu.

Kusoma sura kamili Yn. 7