Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 6:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Baada ya hayo Yesu alikwenda zake ng’ambo ya Bahari ya Galilaya, nayo ndiyo ya Tiberia.

2. Na mkutano mkuu wakamfuata, kwa sababu waliziona ishara alizowafanyia wagonjwa.

3. Naye Yesu akakwea mlimani, akaketi huko pamoja na wanafunzi wake.

4. Na Pasaka, sikukuu ya Wayahudi, ilikuwa karibu.

5. Basi Yesu alipoinua macho yake akaona mkutano mkuu wanakuja kwake, alimwambia Filipo, Tununue wapi mikate, ili hawa wapate kula?

6. Na hilo alilinena ili kumjaribu; kwa maana alijua mwenyewe atakalotenda.

Kusoma sura kamili Yn. 6