Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 4:32-39 Swahili Union Version (SUV)

32. Akawaambia, Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.

33. Basi wanafunzi wake wakasemezana, Je! Mtu amemletea chakula?

34. Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake.

35. Hamsemi ninyi, Bado miezi minne, ndipo yaja mavuno? Tazama, mimi nawaambieni, Inueni macho yenu myatazame mashamba, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno.

36. Naye avunaye hupokea mshahara, na kukusanya matunda kwa uzima wa milele, ili yeye apandaye na yeye avunaye wapate kufurahi pamoja.

37. Kwa maana hapo neno hilo huwa kweli, Mmoja hupanda akavuna mwingine.

38. Mimi naliwatuma myavune yale msiyoyataabikia; wengine walitaabika, nanyi mmeingia katika taabu yao.

39. Na katika mji ule Wasamaria wengi walimwamini kwa sababu ya neno la yule mwanamke, aliyeshuhudia kwamba, Aliniambia mambo yote niliyoyatenda.

Kusoma sura kamili Yn. 4