Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 4:29-37 Swahili Union Version (SUV)

29. Njoni, mtazame mtu aliyeniambia mambo yote niliyoyatenda. Je! Haimkini huyu kuwa ndiye Kristo?

30. Basi wakatoka mjini, wakamwendea.

31. Huko nyuma wanafunzi wakamsihi wakisema, Rabi, ule.

32. Akawaambia, Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.

33. Basi wanafunzi wake wakasemezana, Je! Mtu amemletea chakula?

34. Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake.

35. Hamsemi ninyi, Bado miezi minne, ndipo yaja mavuno? Tazama, mimi nawaambieni, Inueni macho yenu myatazame mashamba, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno.

36. Naye avunaye hupokea mshahara, na kukusanya matunda kwa uzima wa milele, ili yeye apandaye na yeye avunaye wapate kufurahi pamoja.

37. Kwa maana hapo neno hilo huwa kweli, Mmoja hupanda akavuna mwingine.

Kusoma sura kamili Yn. 4