Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 4:25-34 Swahili Union Version (SUV)

25. Yule mwanamke akamwambia, Najua ya kuwa yuaja Masihi, (aitwaye Kristo); naye atakapokuja, yeye atatufunulia mambo yote.

26. Yesu akamwambia, Mimi ninayesema nawe, ndiye.

27. Mara hiyo wakaja wanafunzi wake, wakastaajabu kwa sababu alikuwa akisema na mwanamke; lakini hakuna aliyesema, Unatafuta nini? Au, Mbona unasema naye?

28. Basi yule mwanamke akauacha mtungi wake, akaenda zake mjini, akawaambia watu,

29. Njoni, mtazame mtu aliyeniambia mambo yote niliyoyatenda. Je! Haimkini huyu kuwa ndiye Kristo?

30. Basi wakatoka mjini, wakamwendea.

31. Huko nyuma wanafunzi wakamsihi wakisema, Rabi, ule.

32. Akawaambia, Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.

33. Basi wanafunzi wake wakasemezana, Je! Mtu amemletea chakula?

34. Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake.

Kusoma sura kamili Yn. 4