Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 4:10-19 Swahili Union Version (SUV)

10. Yesu akajibu, akamwambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, ungalimwomba yeye, naye angalikupa maji yaliyo hai.

11. Yule mwanamke akamwambia, Bwana, huna kitu cha kutekea, na kisima ni kirefu; basi umeyapata wapi hayo maji yaliyo hai?

12. Je! Wewe u mkubwa kuliko baba yetu, Yakobo, aliyetupa kisima hiki, naye mwenyewe akanywa maji yake, na wanawe pia, na wanyama wake?

13. Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;

14. walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.

15. Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka.

16. Yesu akamwambia, Nenda kamwite mumeo, uje naye hapa.

17. Yule mwanamke akajibu, akasema, Sina mume. Yesu akamwambia, Umesema vema, Sina mume;

18. kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema kweli.

19. Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii!

Kusoma sura kamili Yn. 4