Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 3:7-12 Swahili Union Version (SUV)

7. Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili.

8. Upepo huvuma upendako, na sauti yake waisikia, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda; kadhalika na hali yake kila mtu aliyezaliwa kwa Roho.

9. Nikodemo akajibu, akamwambia, Yawezaje kuwa mambo haya?

10. Yesu akajibu, akamwambia, Je! Wewe u mwalimu wa Israeli, na mambo haya huyafahamu?

11. Amin, amin, nakuambia kwamba, Lile tulijualo twalinena, na lile tuliloliona twalishuhudia; wala ushuhuda wetu hamwukubali.

12. Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni?

Kusoma sura kamili Yn. 3