Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 2:23-25 Swahili Union Version (SUV)

23. Hata alipokuwapo Yerusalemu kwenye sikukuu wakati wa Pasaka, watu wengi waliamini jina lake, walipoziona ishara zake alizozifanya.

24. Lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote;

25. na kwa sababu hakuwa na haja ya mtu kushuhudia habari za mwanadamu; kwa maana yeye mwenyewe alijua yaliyomo ndani ya mwanadamu.

Kusoma sura kamili Yn. 2