Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 19:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Basi ndipo Pilato alipomtwaa Yesu, akampiga mijeledi.

2. Nao askari wakasokota taji ya miiba, wakamtia kichwani, wakamvika vazi la zambarau.

3. Wakawa wakimwendea, wakisema, Salamu! Mfalme wa Wayahudi! Wakampiga makofi.

4. Kisha Pilato akatokea tena nje, akawaambia, Mtu huyu namleta nje kwenu, mpate kufahamu ya kuwa mimi sioni hatia yo yote kwake.

5. Ndipo Yesu alipotoka nje, naye amevaa ile taji ya miiba, na lile vazi la zambarau. Pilato akawaambia, Tazama, mtu huyu!

Kusoma sura kamili Yn. 19