Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 16:8-13 Swahili Union Version (SUV)

8. Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu.

9. Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi;

10. kwa habari ya haki, kwa sababu mimi naenda zangu kwa Baba, wala hamnioni tena;

11. kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.

12. Hata bado nikali ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili hivi sasa.

13. Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.

Kusoma sura kamili Yn. 16