Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 15:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.

2. Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa.

3. Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia.

4. Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu.

5. Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.

6. Mtu asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka; watu huyakusanya na kuyatupa motoni yakateketea.

Kusoma sura kamili Yn. 15