Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 14:3-9 Swahili Union Version (SUV)

3. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.

4. Nami niendako mwaijua njia.

5. Tomaso akamwambia, Bwana, sisi hatujui uendako; nasi twaijuaje njia?

6. Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.

7. Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona.

8. Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha.

9. Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba?

Kusoma sura kamili Yn. 14