Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 13:24-34 Swahili Union Version (SUV)

24. Basi Simoni Petro akampungia mkono, akamwambia, Uliza, ni nani amtajaye?

25. Basi yeye, hali akimwelekea Yesu kifua chake, akamwambia, Bwana, ni nani?

26. Basi Yesu akajibu, Ndiye mtu yule nitakayemtowelea tonge na kumpa. Akatowelea tonge, akalitwaa akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskariote.

27. Na baada ya hilo tonge Shetani alimwingia. Basi Yesu akamwambia, Uyatendayo yatende upesi.

28. Wala hakuna mtu katika wale walioketi chakulani aliyeijua sababu ya kumwambia hivyo.

29. Kwa maana wengine walidhania, kwa kuwa Yuda huchukua mfuko, ya kwamba Yesu alimwambia kama, Nunua mnavyovihitaji kwa sikukuu; au kwamba awape maskini kitu.

30. Basi huyo, akiisha kulipokea lile tonge, akatoka mara hiyo. Nako kulikuwa ni usiku.

31. Basi huyo alipokwisha kutoka, Yesu alisema, Sasa ametukuzwa Mwana wa Adamu, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.

32. Mungu naye atamtukuza ndani ya nafsi yake; naye atamtukuza mara.

33. Enyi watoto wadogo, bado kitambo kidogo nipo pamoja nanyi; mtanitafuta; na kama vile nilivyowaambia Wayahudi ya kwamba, Mimi niendako ninyi hamwezi kuja; kadhalika sasa nawaambia ninyi.

34. Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.

Kusoma sura kamili Yn. 13