Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 13:14-17 Swahili Union Version (SUV)

14. Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu, nimewatawadha miguu, imewapasa vivyo kutawadhana miguu ninyi kwa ninyi.

15. Kwa kuwa nimewapa kielelezo; ili kama mimi nilivyowatendea, nanyi mtende vivyo.

16. Amin, amin, nawaambia ninyi, Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake; wala mtume si mkuu kuliko yeye aliyempeleka.

17. Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda.

Kusoma sura kamili Yn. 13