Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 12:40-44 Swahili Union Version (SUV)

40. Amewapofusha macho,Ameifanya mizito mioyo yao;Wasije wakaona kwa macho yao,Wakafahamu kwa mioyo yao,Wakaongoka, nikawaponya.

41. Maneno hayo aliyasema Isaya, kwa kuwa aliuona utukufu wake, akataja habari zake.

42. Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi.

43. Kwa maana walipenda utukufu wa wanadamu kuliko utukufu wa Mungu.

44. Naye Yesu akapaza sauti, akasema, Yeye aniaminiye mimi, haniamini mimi bali yeye aliyenipeleka.

Kusoma sura kamili Yn. 12