Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 12:35-40 Swahili Union Version (SUV)

35. Basi Yesu akawaambia, Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako.

36. Maadamu mnayo nuru, iaminini nuru hiyo, ili mpate kuwa wana wa nuru.Hayo aliyasema Yesu, akaenda zake, akajificha wasimwone.

37. Walakini ajapokuwa amefanya ishara nyingi namna hiyo mbele yao, hawakumwamini;

38. ili litimie lile neno la nabii Isaya alilolisema,Bwana, ni nani aliyezisadiki habari zetu;Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?

39. Ndiyo sababu wao hawakuweza kusadiki; kwa maana Isaya alisema tena,

40. Amewapofusha macho,Ameifanya mizito mioyo yao;Wasije wakaona kwa macho yao,Wakafahamu kwa mioyo yao,Wakaongoka, nikawaponya.

Kusoma sura kamili Yn. 12