Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 12:30-40 Swahili Union Version (SUV)

30. Yesu akajibu, akasema, Sauti hiyo haikuwako kwa ajili yangu, bali kwa ajili yenu.

31. Sasa hukumu ya ulimwengu huu ipo; sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje.

32. Nami nikiinuliwa juu ya nchi, nitawavuta wote kwangu.

33. Aliyanena hayo akionyesha ni mauti gani atakayokufa.

34. Basi mkutano wakamjibu, Sisi tumesikia katika torati ya kwamba Kristo adumu hata milele; nawe wasemaje ya kwamba imempasa Mwana wa Adamu kuinuliwa? Huyu Mwana wa Adamu ni nani?

35. Basi Yesu akawaambia, Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako.

36. Maadamu mnayo nuru, iaminini nuru hiyo, ili mpate kuwa wana wa nuru.Hayo aliyasema Yesu, akaenda zake, akajificha wasimwone.

37. Walakini ajapokuwa amefanya ishara nyingi namna hiyo mbele yao, hawakumwamini;

38. ili litimie lile neno la nabii Isaya alilolisema,Bwana, ni nani aliyezisadiki habari zetu;Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?

39. Ndiyo sababu wao hawakuweza kusadiki; kwa maana Isaya alisema tena,

40. Amewapofusha macho,Ameifanya mizito mioyo yao;Wasije wakaona kwa macho yao,Wakafahamu kwa mioyo yao,Wakaongoka, nikawaponya.

Kusoma sura kamili Yn. 12