Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 12:1-14 Swahili Union Version (SUV)

1. Basi, siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alifika Bethania, alipokuwapo Lazaro, yeye ambaye Yesu alimfufua katika wafu.

2. Basi wakamwandalia karamu huko; naye Martha akatumikia; na Lazaro alikuwa mmojawapo wa wale walioketi chakulani pamoja naye.

3. Basi Mariamu akatwaa ratli ya marhamu ya nardo safi yenye thamani nyingi, akampaka Yesu miguu, akamfuta miguu kwa nywele zake. Nayo nyumba pia ikajaa harufu ya marhamu.

4. Basi Yuda Iskariote, mmojawapo wa wanafunzi wake, ambaye ndiye atakaye kumsaliti, akasema,

5. Mbona marhamu hii haikuuzwa kwa dinari mia tatu, wakapewa maskini?

6. Naye aliyasema hayo, si kwa kuwahurumia maskini; bali kwa kuwa ni mwivi, naye ndiye aliyeshika mfuko, akavichukua vilivyotiwa humo.

7. Basi Yesu alisema, Mwache aiweke kwa siku ya maziko yangu.

8. Kwa maana maskini mnao sikuzote pamoja nanyi; bali mimi hamnami sikuzote.

9. Basi watu wengi katika Wayahudi walipata kujua ya kuwa yeye yuko huko, nao wakaja, si kwa ajili yake Yesu tu, ila wamwone na Lazaro, ambaye Yesu alimfufua katika wafu.

10. Nao wakuu wa makuhani wakafanya shauri la kumwua Lazaro naye;

11. maana kwa ajili yake wengi katika Wayahudi walijitenga, wakamwamini Yesu.

12. Nayo siku ya pili yake watu wengi walioijia sikukuu walisikia ya kwamba Yesu anakuja Yerusalemu;

13. wakatwaa matawi ya mitende, wakatoka nje kwenda kumlaki, wakapiga makelele, Hosana! Ndiye mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana, Mfalme wa Israeli!

14. Naye Yesu alikuwa amepata mwana-punda, akampanda, kama vile iliyoandikwa,

Kusoma sura kamili Yn. 12