Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 11:8-19 Swahili Union Version (SUV)

8. Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, juzijuzi tu Wayahudi walikuwa wakitafuta kukupiga kwa mawe, nawe unakwenda huko tena?

9. Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.

10. Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake.

11. Aliyasema hayo; kisha, baada ya hayo, akawaambia, Rafiki yetu, Lazaro, amelala; lakini ninakwenda nipate kumwamsha.

12. Basi wale wanafunzi wakamwambia, Bwana, ikiwa amelala, atapona.

13. Lakini Yesu alikuwa amenena habari ya mauti yake; nao walidhania ya kuwa ananena habari ya kulala usingizi.

14. Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.

15. Nami nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini; lakini na twendeni kwake.

16. Basi Tomaso, aitwaye Pacha, akawaambia wanafunzi wenziwe, Twendeni na sisi, ili tufe pamoja naye.

17. Basi Yesu alipofika, alimkuta amekwisha kuwamo kaburini yapata siku nne.

18. Na Bethania ilikuwa karibu na Yerusalemu, kadiri ya maili mbili hivi;

19. na watu wengi katika Wayahudi walikuwa wamekuja kwa Martha na Mariamu, ili kuwafariji kwa habari ya ndugu yao.

Kusoma sura kamili Yn. 11