Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 11:7-15 Swahili Union Version (SUV)

7. Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, Twendeni Uyahudi tena.

8. Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, juzijuzi tu Wayahudi walikuwa wakitafuta kukupiga kwa mawe, nawe unakwenda huko tena?

9. Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.

10. Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake.

11. Aliyasema hayo; kisha, baada ya hayo, akawaambia, Rafiki yetu, Lazaro, amelala; lakini ninakwenda nipate kumwamsha.

12. Basi wale wanafunzi wakamwambia, Bwana, ikiwa amelala, atapona.

13. Lakini Yesu alikuwa amenena habari ya mauti yake; nao walidhania ya kuwa ananena habari ya kulala usingizi.

14. Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.

15. Nami nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini; lakini na twendeni kwake.

Kusoma sura kamili Yn. 11