Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 11:4-8 Swahili Union Version (SUV)

4. Naye Yesu aliposikia, alisema, Ugonjwa huu si wa mauti, bali ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu, ili Mwana wa Mungu atukuzwe kwa huo.

5. Naye Yesu alimpenda Martha na umbu lake na Lazaro.

6. Basi aliposikia ya kwamba hawezi, alikaa bado siku mbili pale pale alipokuwapo.

7. Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, Twendeni Uyahudi tena.

8. Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, juzijuzi tu Wayahudi walikuwa wakitafuta kukupiga kwa mawe, nawe unakwenda huko tena?

Kusoma sura kamili Yn. 11