Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 11:2-17 Swahili Union Version (SUV)

2. Ndiye Mariamu yule aliyempaka Bwana marhamu, akamfuta miguu kwa nywele zake, ambaye Lazaro nduguye alikuwa hawezi.

3. Basi wale maumbu wakatuma ujumbe kwake wakisema, Bwana, yeye umpendaye hawezi.

4. Naye Yesu aliposikia, alisema, Ugonjwa huu si wa mauti, bali ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu, ili Mwana wa Mungu atukuzwe kwa huo.

5. Naye Yesu alimpenda Martha na umbu lake na Lazaro.

6. Basi aliposikia ya kwamba hawezi, alikaa bado siku mbili pale pale alipokuwapo.

7. Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, Twendeni Uyahudi tena.

8. Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, juzijuzi tu Wayahudi walikuwa wakitafuta kukupiga kwa mawe, nawe unakwenda huko tena?

9. Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.

10. Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake.

11. Aliyasema hayo; kisha, baada ya hayo, akawaambia, Rafiki yetu, Lazaro, amelala; lakini ninakwenda nipate kumwamsha.

12. Basi wale wanafunzi wakamwambia, Bwana, ikiwa amelala, atapona.

13. Lakini Yesu alikuwa amenena habari ya mauti yake; nao walidhania ya kuwa ananena habari ya kulala usingizi.

14. Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.

15. Nami nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini; lakini na twendeni kwake.

16. Basi Tomaso, aitwaye Pacha, akawaambia wanafunzi wenziwe, Twendeni na sisi, ili tufe pamoja naye.

17. Basi Yesu alipofika, alimkuta amekwisha kuwamo kaburini yapata siku nne.

Kusoma sura kamili Yn. 11