Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 11:18-29 Swahili Union Version (SUV)

18. Na Bethania ilikuwa karibu na Yerusalemu, kadiri ya maili mbili hivi;

19. na watu wengi katika Wayahudi walikuwa wamekuja kwa Martha na Mariamu, ili kuwafariji kwa habari ya ndugu yao.

20. Basi Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alikwenda kumlaki; na Mariamu alikuwa akikaa nyumbani.

21. Basi Martha akamwambia Yesu, Bwana, kama ungalikuwapo hapa, ndugu yangu hangalikufa.

22. Lakini hata sasa najua ya kuwa yo yote utakayomwomba Mungu, Mungu atakupa.

23. Yesu akamwambia, Ndugu yako atafufuka.

24. Martha akamwambia, Najua ya kuwa atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.

25. Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi;

26. naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo?

27. Akamwambia, Naam, Bwana, mimi nimesadiki ya kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni.

28. Naye alipokwisha kusema hayo, alikwenda zake; akamwita umbu lake Mariamu faraghani, akisema, Mwalimu yupo anakuita.

29. Naye aliposikia, aliondoka upesi, akamwendea.

Kusoma sura kamili Yn. 11