11. Aliyasema hayo; kisha, baada ya hayo, akawaambia, Rafiki yetu, Lazaro, amelala; lakini ninakwenda nipate kumwamsha.
12. Basi wale wanafunzi wakamwambia, Bwana, ikiwa amelala, atapona.
13. Lakini Yesu alikuwa amenena habari ya mauti yake; nao walidhania ya kuwa ananena habari ya kulala usingizi.
14. Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.