Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 10:24-29 Swahili Union Version (SUV)

24. Basi Wayahudi walimzunguka, wakamwambia, Hata lini utatuhangaisha nafsi zetu? Kama wewe ndiwe Kristo, utuambie waziwazi.

25. Yesu akawajibu, Naliwaambia, lakini ninyi hamsadiki. Kazi hizi ninazozifanya kwa jina la Baba yangu ndizo zinazonishuhudia.

26. Lakini ninyi hamsadiki, kwa sababu hammo miongoni mwa kondoo wangu.

27. Kondoo wangu waisikia sauti yangu; nami nawajua, nao wanifuata.

28. Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu.

29. Baba yangu aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote; wala hakuna mtu awezaye kuwapokonya katika mkono wa Baba yangu.

Kusoma sura kamili Yn. 10