Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 10:17-23 Swahili Union Version (SUV)

17. Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena.

18. Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu.

19. Kukaingia tena matengano kati ya Wayahudi, kwa ajili ya maneno hayo.

20. Wengi wao wakasema, Ana pepo huyu, tena ana wazimu; mbona mnamsikiliza?

21. Wengine wakasema, Maneno hayo siyo ya mtu mwenye pepo. Je! Pepo aweza kuwafumbua macho vipofu?

22. Basi huko Yerusalemu ilikuwa Sikukuu ya Kutabaruku; ni wakati wa baridi.

23. Naye Yesu alikuwa akitembea hekaluni, katika ukumbi wa Sulemani.

Kusoma sura kamili Yn. 10