Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 10:15-24 Swahili Union Version (SUV)

15. kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo.

16. Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; na sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.

17. Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena.

18. Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu.

19. Kukaingia tena matengano kati ya Wayahudi, kwa ajili ya maneno hayo.

20. Wengi wao wakasema, Ana pepo huyu, tena ana wazimu; mbona mnamsikiliza?

21. Wengine wakasema, Maneno hayo siyo ya mtu mwenye pepo. Je! Pepo aweza kuwafumbua macho vipofu?

22. Basi huko Yerusalemu ilikuwa Sikukuu ya Kutabaruku; ni wakati wa baridi.

23. Naye Yesu alikuwa akitembea hekaluni, katika ukumbi wa Sulemani.

24. Basi Wayahudi walimzunguka, wakamwambia, Hata lini utatuhangaisha nafsi zetu? Kama wewe ndiwe Kristo, utuambie waziwazi.

Kusoma sura kamili Yn. 10