Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 1:8-20 Swahili Union Version (SUV)

8. Huyo hakuwa ile nuru, bali alikuja ili aishuhudie ile nuru.

9. Kulikuwako Nuru halisi, amtiaye nuru kila mtu, akija katika ulimwengu.

10. Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukumtambua.

11. Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea.

12. Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;

13. waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.

14. Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.

15. Yohana alimshuhudia, akapaza sauti yake akasema, Huyu ndiye niliyenena habari zake ya kwamba, Ajaye nyuma yangu amekuwa mbele yangu; kwa maana alikuwa kabla yangu.

16. Kwa kuwa katika utimilifu wake sisi sote tulipokea, na neema juu ya neema.

17. Kwa kuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa; neema na kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo.

18. Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua.

19. Na huu ndio ushuhuda wake Yohana, Wayahudi walipotuma kwake makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamwulize, Wewe u nani?

20. Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye Kristo.

Kusoma sura kamili Yn. 1